SERIKALI ya Rais John Magufuli inaelezwa kuendeshwa kwa woga na hofu ya kuumbuliwa hasa kwenye mijadala mikali ya Bunge,
Hatua hiyo inaelezwa kuisukuma serikali kufikia uamuzi wa kuzuia kurusha moja kwa moja matangazo ya Bunge la Jamhuri kupitia Televisheni ya Shirika la Utangazaji nchini (TBC) na pia uamuzi huo kuelekezwa kwenye televisheni binafsi jambo ambalo linaelezwa kuminya uhuru wa habari.
Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimekuwa vikiitaka serikali kuachana na mpango huo kwa kuwa, vinavyima haki ya wananchi kupata habari jambo ambalo huwasaidia kufanya maamuzi sahihi.
Abdul Kambaya, Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, Chama cha Wananchi (CUF) – miongoni mwa vyama vya Ukawa- amesema, Serikali ya Rais Magufuli ina hofu kutokana na mijadala ambayo inaweza kuibuliwa na wapinzani na serikali kushindwa kutoa majibu yanayoeleweka.
“Baada ya kuingia madarakani, Serikali ya Awamu ya Tano kulikuwa na mabadiliko ikiwemo kuminywa kwa uhuru wa habari, yaani kupata na kueneza habari,” amesema Kambaya na kuongeza;
“Bunge linapooneshwa moja kwa moja, linawejenga wananchi na kuwaonesha jinsi serikali yao inavyowajibika pamoja na kufuatilia miradi mbalimbali ya maendeleo inayojadiliwa bungeni.”
Januari mwaka huu Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo aliwasilisha taarifa ya serikali ya kuzuia TBC kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge la Jamhuri kwa madai ya gharama kubwa za urushwaji wa matangazo hayo.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
Post A Comment: