ads
 
SERIKALI ya Rais John Magufuli inaelezwa kuendeshwa kwa woga na hofu ya kuumbuliwa hasa kwenye mijadala mikali ya Bunge,


    Hatua hiyo inaelezwa kuisukuma serikali kufikia uamuzi wa kuzuia kurusha moja kwa moja matangazo ya Bunge la Jamhuri kupitia Televisheni ya Shirika la Utangazaji nchini (TBC) na pia uamuzi huo kuelekezwa kwenye televisheni binafsi jambo ambalo linaelezwa kuminya uhuru wa habari.

Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimekuwa vikiitaka serikali kuachana na mpango huo kwa kuwa, vinavyima haki ya wananchi kupata habari jambo ambalo huwasaidia kufanya maamuzi sahihi.

Abdul Kambaya, Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, Chama cha Wananchi (CUF) – miongoni mwa vyama vya Ukawa- amesema, Serikali ya Rais Magufuli ina hofu kutokana na mijadala ambayo inaweza kuibuliwa na wapinzani na serikali kushindwa kutoa majibu yanayoeleweka.

“Baada ya kuingia madarakani, Serikali ya Awamu ya Tano kulikuwa na mabadiliko ikiwemo kuminywa kwa uhuru wa habari, yaani kupata na kueneza habari,” amesema Kambaya na kuongeza;

“Bunge linapooneshwa moja kwa moja, linawejenga wananchi na kuwaonesha jinsi serikali yao inavyowajibika pamoja na kufuatilia miradi mbalimbali ya maendeleo inayojadiliwa bungeni.”

Januari mwaka huu Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo aliwasilisha taarifa ya serikali ya kuzuia TBC kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge la Jamhuri kwa madai ya gharama kubwa za urushwaji wa matangazo hayo.


DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: