Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jana ijumaa Novemba 24 2017, imeahirisha kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Singh Sethi na mfanyabiashara, James Rugemarila hadi Desemba 8, 2017, kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika.


Upande wa mashtaka umemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa wanaomba upelelezi ukamilike kwa haraka kwasababu hali ya mshtakiwa mmoja si nzuri.

Harbinder Singh Sethi pamoja na Mfanyabiashara James Rugemarila, kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya zaidi ya Bilioni 3.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: