Mshambuliaji Saimon Msuva alifunga bao la ufundi mkubwa wakati timu yake Difaa El Jadida ikikubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Wydad Casablanca ugenini katika mchezo wa Ligi Kuu Morocco ‘Batola Pro’.


Msuva alifunga bao lake akiunganisha kwa shuti la moja kwa moja mpira kichwa uliopigwa na beki wa Wydad aliyejaribu kuokoa mpira huo.

Mshambuliaji huyo amekuwa na mafanikio makubwa tangu alipotua El Jadida akitokea Yanga mwisho wa msimu uliopita.

Mabadiliko yaliyofanywa na kocha mkuu wa Difaa, Abderrahim Talib baada ya kuongozwa kwa mabao 2-0  kwa kuwatoa  Mario Mandrault, Bilal El Magri na nafasi zao kuchukuliwa na Tarik Astati, Hamid Ahadad  yalionekana kuwa na tija kwa Msuva kufunga bao la kufutia machozi.

Hicho ni kipigo cha pili kwa Msuva kukipata ndani ya siku tano baada ya kufungwa kwa penalty 3-1 mwishoni mwa wiki katika Kombe la Mfalme dhidi ya Raja Casablanca.

Difaa itacheza tena  ugenini, Novemba  26 kwenye uwanja wa  Stade Père-Jégo (Casablanca) na wenyeji wao, Racing de  Casablanca, majira ya saa 12;00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: