
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KLABU za Gor Mahia inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya na St. George ya Ethiopia, zinatajwa kumwania mshambuliaji wa kimataifa wa Simba kutoka Burundi, Laudit Mavugo, imeelezwa.
Hata hivyo, Akizungumza na gazeti la Nipashe jana, Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah "Try Again" amesema kuwa hakuna mchezaji hata mmoja atakayeachwa na hiyo inatokana na ripoti ya kiufundi waliyokabidhiwa na Kocha Mkuu, Joseph Omog.
Salim alisema jana kuwa chini ya uongozi wake, hakutakuwa na kiongozi atakayesajili mchezaji au atakayependekeza nyota kuachwa, kwa sababu jukumu hilo liko chini ya Omog na wasaidizi wake tu.
"Kila kitu kinaendeshwa kwa kufuata kanuni na taratibu, Simba ni taasisi na ni kubwa kuliko mchezaji au kiongozi, ni lazima hilo liheshimiwe," alisema kiongozi huyo ambaye anakaimu nafasi iliyoachwa na Evans Aveva, anatuhumiwa kutumia vibaya fedha za klabu.
Taarifa zilizopatikana jijini zinasema kuwa kuna mazungumzo yasiyo rasmi yanaendelea na lengo la kufanya hivyo ni kutaka kushawishi mshambuliaji huyo aachwe kwa ajili ya kukwepa kulipa ada ya uhamisho kwa sababu mshambuliaji huyo bado ana mkataba na Simba.
"Mimi najua St. George ndiyo wanamtaka, na hawakuanza sasa, ila wanaonyesha wanataka kumsajili kupitia mlango wa nyuma, na hili haliwezekani," alisema kiongozi mmoja wa Simba.
Post A Comment: