
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba amesema hatakuwa na sababu ya kuendelea kuwa waziri endapo Watanzania watakosa ugali juu ya meza.
Dk Tizeba amesema hayo jana Alhamisi wakati wa mkutano wa saba wa baraza la nafaka la ukanda wa Afrika Mashariki (EAGC).
Amesema Serikali itaendelea na jukumu la kuhakikisha chakula kinakuwepo nchini.
Waziri amesema mwanzoni mwa mwaka huu baadhi ya wabunge na vyombo vya habari vilimshinikiza atangaze uwepo wa njaa nchini lakini hakufanya hivyo kwa sababu hapakuwa na njaa.
"Siko kwenye nafasi ya kutangaza njaa lakini nisingemshauri Rais kufanya hivyo kwa kuwa licha ya mavuno kidogo yaliyokuwepo kipindi kile, Serikali inaamini watu walikuwa na chakula cha kutosha," amesema Dk Tizeba.
Amesema hata yeye angekuwa Rais asingeweza kutangaza njaa kwa kuwa hali hiyo ilitokea ikiwa ni miezi miwili tu tangu wafanyabiashara waishinikize Serikali kutoa vibali vya kuuza nafaka nje ya nchi.
"Isingewezekana njaa kuja ghafla. Kitendo cha wafanyabiashara kutaka ruksa ya kuuza mazao nje kilimaanisha chakula kilikuwepo cha ziada," amesema Dk Tizeba.
Hata hivyo, Dk Tizeba amesema hali ya chakula kwa mwaka huu imepungua kwa asilimia tatu kulinganisha na mwaka jana.
Kutokana na hilo, amesema chakula kinapaswa kutumika vizuri kuepuka upungufu.
Post A Comment: