ads

Je, umeshawahi kula mchele feki wa plastic toka China? Wajua madhara yake?


Hawa wachina huku walikofikia sasa ni kuimaliza dunia. Kuna mchele unaitwa Milagrosa Dyne Super Rice ambao unasambazwa toka China. Mchele huu ambao umethibitika kuwa una madhara katika mwili wa binadamu. Mchele huo unatengenezwa kwa kutumia chemikali kali zinazotengeneza plastic.

Kwa kifupi mchele huo ni wa plastic na haufai kwa kula. Huwezi kuutambua kwa macho zaidi ya kuuloweka kwenye maji. Mchele huo ukilowekwa kwenye maji unachukua muda kiasi kuzama katika maji na kulowana. Mchele huo ulianza kusambaa nchi za Sudan, somalia na Ethiopia kipindi kile cha njaa. Na sasa inasemekana mchele huo huenda upo ama ukaanza kuuzwa tanzania pia.

Mchele huo una madhara mengi katika mwili wa binadamu ikiwa ni pamoja na kutengeneza kansa ya mishipa ya damu na kuharibu mfumo mzima wa mzunguko wa chembe chembe nyeupe mwilini ambayo kwa baadae mwili huvimba na kuanza kutoa wadudu wa ajabu ajabu kama funza mwilini.


Inachukua takribani miezi tisa kugundua una tatizo hilo kwani wale wadudu hukua taratibu sana na sio rahisi kuwaona wala kuwahisi mpaka wanapokuwa wakubwa na kuanza kukutembea mwilini na eneo walipojipenyeza huvimba kama jipu.

Kuweni makini sana mnapoenda kwenda kwenye ma-supper market kununua bidhaa ama mchele toka nje za nchi. Mtakula na visivyoliwa.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: