
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
IGP Sirro, amefanya mabadiliko katika jeshi la polisi ili kuboresha utendaji wa jeshi hilo kwa kumuhamisha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Mohamed Mpinga na kuwa Kamanda wa polisi wa mkoa Mbeya
Katika taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi inasema kuwa aliyekuwa Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya (DCP) Dhahiri Kidavashari amehamishiwa Makao Makuu ya upelelezi.
Kufuatia mabadiliko hayo nafasi aliyokuwa nayo Mohamed Mpinga imechukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Fortunatus Musilimu.
Kwa mujibu wa Barnabas Mwakalukwa (ACP) ambaye ni msemaji wa jeshi la polisi, Makao Makuu ya Jeshi hilo amesema uhamisho huo ni wa kawaida katika kuboresha utendaji wa kazi za Polisi kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.
IGP Saimon Sirro alishauriwa na Rais John Pombe Magufuli kufanya mabadiliko katika jeshi hilo ili kuleta ufanisi na kuboresha utendaji wa jeshi la polisi nchini, jambo ambalo tayari inaonyesha ameanza kulifanyia kazi kwa kufanya mabadiliko kama haya.
Post A Comment: