
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KIKOHOZI ni ugonjwa unaowapata watu karibu wote, hali ya muwasho kooni pamoja na kuziba kwa baadhi ya sehemu za kupumulia puani, ubongo hutambua kuwa kuna hitilafu katika mwili.
Kukohoa pia kunaweza kuwa ni matokeo ya maambukizi ya virusi, homa, kuvuta sigara au matatizo ya kiafya kama pumu, kifua kikuu na kansa ya mapafu.
Baadhi ya dalili za kikohozi ni muwasho kooni, maumivu ya kifua na msongamano mapafuni.
Badala ya kutumia dawa za viwandani kutibu kikohozi, unaweza kujaribu mojawapo ya hizi dawa za asili za kikohozi ambazo zinapatikana kirahisi jikoni kwako.
Binzari (Turmeric)
Dawa hii ya asili inao uwezo wa kutibu kikohozi, hasa kikohozi kikavu.
Weka kijiko kidogo kimoja cha unga wa binzari ndani ya kikombe kimoja (robo lita) cha maji ya moto, ongeza ndani kijiko kidogo cha pilipili manga ya unga.
Nusu kijiko cha chai cha unga wa mdalasini na kijiko kidogo kimoja cha asali mbichi, koroga vizuri na unywe mchanganyiko huu wote kutwa mara moja kila siku mpaka umepona.
2. Tangawizi
Tangawizi ni moja ya dawa maarufu kwa kutibu kikohozi.
Tengeneza chai ukitumia tangawizi mbichi na ndani yake utumie asali na siyo sukari kwenye hii chai yako.
Kunywa kikombe kimoja kutwa mara 3 kila siku mpaka utakapopona.
Angalizo, usitumie dawa hii kama una ujauzito mchanga chini ya miezi minne na hata ukiwa na ujauzito zaidi ya miezi minne basi tumia kikombe kimoja tu kwa siku.
Unaweza pia kutengeneza juisi ya tangawizi freshi ukiongeza parachichi ndani yake na unywe kwa mtindo huo huo wa chai hapo juu.
Limau
Limau linaweza kutumika kwa namna nyingi katika kutibu kikohozi.
Limau zina sifa za kuondoa maambukizi, pia lina vitamini muhimu ambayo hupigana na maambukizi na kukuongezea kinga ya mwili, vitamini mhimu sana, vitamini C.
Changanya vijiko vikubwa viwili vya maji ya limau na kijiko kikubwa kimoja cha asali mbichi na unywe mchanganyiko huo mara mbili kwa siku ndani ya siku kadhaa.
Post A Comment: