Kampuni ya uchimbaji madini, Acacia (Acacia Mining) imefunguka na kusema kuwa haina uwezo wa kulipa dollar milioni 300 kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kutatua mgogoro wa kodi. 


Akiongea jana Oktoba 20, 2017 kwa njia ya simu na chombo cha habari cha Kimataifa cha Uingereza (Reuters) Afisa wa Fedha wa Acacia, Andrew Wray kampuni hiyo haina uwezo wa kulipa fedha hizo kwa serikali ya Tanzania. 

Washirika wakubwa wa Acacia, Barrick Gold siku ya juzi Oktoba 19 walikubalina na serikali ya Tanzania kuwa watalipa dollar milioni 300 kwa serikali ya Tanzania pamoja na kugawana mapato yanayotokana na shughuli za uchimbaji wa madini nchini.

Chanzo cha habari tovuti ya Reuters.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: