
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Balozi wa China nchini, Lu Youging amempongeza Rais John Magufuli na Serikali kwa bajeti nzuri iliyowasilishwa jana, Juni 8 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango.
Balozi Youging ametoa pongezi hizo jana (Ijumaa) Ikulu jijini hapa alikokwenda kufanya mazungumzo na Rais.
Amesema bajeti hiyo imeakisi dhamira za kuongeza kasi ya maendeleo katika sekta mbalimbali za ikiwamo ya ujenzi na miundombinu.
βLakini pamoja na bajeti nzuri kuwasilishwa uchumi wa Tanzania umeendelea kuimarika na kuwavutia wadau wengi wa maendeleo kuwekeza nchini,β amesema.
Ameongeza kuwa Tanzania inapewa kipaumbele na nchi ya China na kwamba Serikali ya nchi hiyo itaendelea kuwashawishi wawekezaji wengi zaidi kuwekeza hapa nchini.
Post A Comment: