ads

Aliyekuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama cha siasa ACT – Wazalendo, Anna Mghwira amedai Tanzania bado haina uchaguzi wa demokrasia huku akiweka wazi mpango wake wa kugombea ubunge katika uchaguzi ujao wa mwaka 2020 jimbo la Singida.


Mwanamama huyo ambaye alionyesha ujasiri mkubwa katika mbio za kuwania kiti cha Urais katika uchaguzi wa mwaka 2015, amesema hayo Jumatatu hii wakati akizungumza kupitia kipindi Cha Dakika 45 cha ITV.

“Siwazi siioni Tanzania ya uchaguzi ya mwaka 2020. Hatuna chaguzi za demokrasia bado. Pengine naweza kugombea nafasi ya ubunge jimbo la Singida mjini mwaka 2020,” alijibu Mama Anna Mghwira wakati akieleza mipango yake katika uchaguzi ujao.

Katika hatua nyingine Mama Anna aliishauri serikali kuwekeza katika kilimo ili kuiandaa Tanzania ya Viwanda.

“Hatuwezi kuwa na Tanzania ya viwanda bila ya kuboresha kilimo kwanza, Tunahitaji kuwa na Tanzania ya kilimo kwanza,” alimema.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: