ads

Bandeji ambazo zinaweza kutambua jinsi kidonda kinavyopona na kutuma ujumbe kwa daktari itafanyiwa majaribio katika kipindi cha miezi 12 ijayo.


Bandeji hizo zitatumia teknolojia ya 5G kufuatilia na kutambua ni matibabu ya aina gani yanahitajika kwa mgonjwa.

Majaribio hayo yanafanywa na taasisi ya Sayansi ya chuo cha Swansea huko Wales nchini Uingereza.

Bandeji hii inatumia teknolojia inayofahamika kama nano, kutambua hali ya kidonda cha mgonjwa wakati wote.

Kisha itaunganisha kidonda na mfumo wa 5G kupitia kwa simu ya mkononi na kuonyesha vitu kadhaa kuhusu mgonjwa, kama eneo alipo na hali yake.

Wakati taarifa hiyo yote inakuja pamoja, teknolojia hiyo kisha itatambua aina ya matibabu mgonjwa ambayo anahitaji kuyapata.

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: