ads

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema kwamba kuanzia wiki ijayo wizara yake itawatangaza hadharani watu wote ambao wamekwepa kulipa kodi ya ardhi na majengo, wakiwemo vigogo walioko serikalini.


Akifungua semina juu ya jukumu la vyombo vya habari katika kutoa elimu ya sheria, kanuni na taratibu katika utawala wa ardhi ili kusaidia kutatua migogoro, iliyofanyika mjini hapa, Lukuvi alisema kwamba watayatangaza majina hayo ili watu wawajue watu wanaojenga majumba ya kifahari lakini hataki kulipa kodi ya serikali.

“Tutatangaza majina yao halisi sio yale ya bandia, ili watu wawajue kuwa kuna watu wamejenga majumba ya fahari, lakini hawalipi kodi ya serikali, baada ya kutangaza tutawapiga faini. Na mwakani tutaweka kodi kubwa zaidi kwa mashamba na viwanja visivyoendelezwa,” alisema Lukuvi.

Alisema gharama ya kodi, pia imepunguzwa kutoka Sh 1,000 na sasa mtu atalipia ekari moja kwa Sh 400. 

“Nani huyo asiyeweza kulipia kiasi hicho cha fedha,” alihoji.

Alisema wizara yake inaangalia hata wale ambao wanamiliki kimila, nao wachangie kidogo, kwa sasa hawalipii hata kidogo Kuhusu hoja ya kuwanyang’anya watu mashamba ambayo hayajaendelezwa, alisema serikali haitaangalia cheo, jina wala wadhifa wa mtu, badala yake wale wote wenye mashamba ambayo hajaendelezwa watanyang’anywa.

Alisema kama kuna kiongozi yeyote serikali au kigogo mstaafu, ambaye amehodhi ardhi katika mkoa wowote na hajaiendeleza, huyo atahesabiwa amekiuka masharti ya kumilikishwa ardhi na hivyo lazima achang’anywe.

Alisema kabla ya kufuta hati ya umiliki, Serikali inatoa notisi ya kufuta kabla ya kufanya hivyo kwa viwanja na mashamba, sasa mchakato ukiiva baada ya siku 90 kama utetezi wake hauridhishi, anampelekea rais anafuta hati hizo za umiliki.“Hakuna atakayepona katika mpango huu,” alisema Lukuvi.

Alishauri taasisi za serikali kutumia wapima ardhi binafsi kwani ni waadilifu kuliko wale wa serikali, “Wapima binafsi ni waadilifu, mkiwapa kazi maeneo yetu yatapona, mkiwapa viwanja 1,000 watakurudishia viwanja vyote, ila aliyeajiriwa na halmashauri atakurudishia viwanja 500, viwanja 500 ‘atavipiga’. Na ‘upigaji’ wao ni ufundi haswa.”

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: