ads

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema haina mpango wa kuwazuia viongozi wastaafu kugombea urais wa visiwa hivyo pamoja na kwamba wananufaika na mafao ya nyadhifa zao walizokuwa wakizitumikia akiwamo aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad.


Hayo yalisemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi (BLM), Issa Haji Gavu, alipokua akijibu swali la Mwakilishi wa Mfenesini, Machano Othman Said, katika kikao cha Baraza la Wawakilishi jana.

Alisema sheria namba 2 ya 2012 imeanzishwa kwa madhumuni ya kuwaenzi na kuwatunza viongozi wastaafu Zanzibar kwa kutambua mchango wao katika kulitumikia taifa na wananchi wake.

“Sheria hii haikuzungumzia suala la kuwakataza viongozi hao kutogombea nafasi nyengine za uongozi katika serikali kupitia vyama vyao baada ya kustaafu.” 

"Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi lazima mfahamu suala la kuchagua na kuchaguliwa ni haki ya kikatiba kwa kila mwananchi aliyefikia vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa kifungu cha 26 (a) (d) cha Katiba ya Zanzibar ya 1984. 

Wakati huu serikali haioni busara ya kuwabana kisheria viongozi wa kisiasa wastaafu wasitumie fursa yao ya kikatiba kugombea uongozi pale wanapoona inafaa,” alisema Gavu.

Aidha, w
aziri huyo alisema haki ya kuwalipa viongozi wa kisiasa wastaafu ni jambo la kisheria na halitokani na utashi, hivyo serikali itaendelea kuwalipa na kuwapa haki zao nyengine viongozi hao kama sheria ilivyosema.

Pia alisema serikali haina wazo la kuwa na baraza la ushauri la viongozi wastaafu kwani Rais hakwaziki kutaka ushauri kwa mtu yoyote na wala halazimiki kufuata ushauri wa mtu yoyote katika utekelezaji wa majukumu yake.

Viongozi ambao wamestaafu nyadhifa za juu serikalini visiwani hapa na wamekua wakiwania nafasi ya urais wa ni Maalim Seif (CUF) na aliyekuwa Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha (CCM).
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: