idd-1
Klabu ya Simba imeingia mkataba wa mwaka mmoja na kocha wa makipa Iddi Salim Raia wa Kenya ikiwa ni mara yake ya pili kuinoa Simba.
 
Kocha huyu mwenye uzoefu katika kazi yake alitumbuliwa na Simba akiwa pamoja na kocha wa kipindi kile Mwingereza Dylan Kerr baada ya kufanya vibaya hivyo wote walitupiwa virago.
 
Safari hii amerejea Simba akiwa amejifua zaidi na kupata leseni ya Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa), maana yake anaweza kufanya kazi Barani Ulaya.
 
Kocha huyu pia alishawahi kufanya kazi na Mabingwa wa Zamani wa Kenya timu ya Gor Mahia, AFC Leopards za Kenya pamoja na timu ya taifa ya nchini hiyo, Harambee Stars.
 
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: