ads

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa ufafanuzi kuhusu miili 7 ya watu iliyokutwa ikielea katika mto Ruvu na kusema kuwa linaendelea na upelelezi kwa lengo la kuwatambua marehemu hao. 


Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa makosa ya JInai Kamishna wa Polisi Robert Boaz, amesema jeshi hilo bado halijawatambua marehemu hao, huku akitetea uamuzi wa jeshi hilo kuzika haraka miili ya marehemu 6 kati ya 7.
 
"Hatua zote za kitaalam zilifuatwa na tunaendelea kufanya upelelezi unaolenga kuwatambua marehemu hao na kujua ni jambo gani liliwasibu, tunawasihi wananchi kuendelea kutupa taarifa zitakazosaidia kutambulika kwa marehemu hao" Amesema Boaz

Akielezea jinsi jeshi hilo lilivyopata taarifa, amesema jeshi hilo lilipata taarifa za kuelea kwa maiti 7 katika mto Ruvu eneo la Mkuruge wilayani Bagamoyo kati ya tarehe 6/12/2016 hadi 9/12/2016 ambapo askari na daktari walifika katika eneo la tukio na kufanya uchunguzi wa kitaalam.

Amesema miili 6 kati ya 7 ilikuwa imeharibika sana na ndiyo maana iliamuliwa zizikwe katika eneo la tukio wakati moja yenye unafuu ikipelekwa hospitali ya wilaya ya Bagamoyo hadi tarehe 16/12/2016 ilipozikwa na halmashauri baada ya kutotambuliwa na tu yoyote.

Kuhusu kutoweka kwa msaidizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Ben Sanane, Kamishna Boaz amesema jeshi hilo linaendelea na upelelezi ili kubaini mahali alipo na kilichomsibu.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: