KIUNGO wa Yanga, Mnyarwanda, Haruna
Niyonzima, amesema mbinu za kocha wao George Lwandamina zitawafanya
wasishikike baada ya siku chache kuanzia sasa.
Niyonzima
ametoa kauli hiyo siku chache baada ya mchezo wa kwanza wa mzunguko wa
pili wa Ligi Kuu dhidi ya JKT Ruvu ambayo walishinda kwa mabao 3-0.
"Mimi naiona Yanga nyingine, kocha ameongeza mbinu na kutupa makali na hili litaonekana kwenye mzunguko wa pili unaoendelea," alisema Niyonzima.
Alisema kikosi chao kinauwezo wa kufanya vizuri zaidi ya yale waliyoyaonyesha kwenye mchezo uliopita ambao ulichezwa Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Nahodha huyo wa timu ya Taifa ya Rwanda, alisema kama kila mchezaji atafuata wanachofundishwa kwenye mazoezi wananafasi kubwa ya kutetea ubingwa wao.
Niyonzima amerejea kwenye kiwango chake cha juu cha uchezaji ambapo katika mchezo wa juzi alionyesha uwezo mkubwa na kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi huo uliowafanya waendelee kuifukuza kwa karibu Simba inayoongoza ligi.
Timu hizo zimepishana kwa pointi mbili huku Simba ikiongoza kwa pointi 38 baada ya timu zote kucheza michezo 16.
"Mimi naiona Yanga nyingine, kocha ameongeza mbinu na kutupa makali na hili litaonekana kwenye mzunguko wa pili unaoendelea," alisema Niyonzima.
Alisema kikosi chao kinauwezo wa kufanya vizuri zaidi ya yale waliyoyaonyesha kwenye mchezo uliopita ambao ulichezwa Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Nahodha huyo wa timu ya Taifa ya Rwanda, alisema kama kila mchezaji atafuata wanachofundishwa kwenye mazoezi wananafasi kubwa ya kutetea ubingwa wao.
Niyonzima amerejea kwenye kiwango chake cha juu cha uchezaji ambapo katika mchezo wa juzi alionyesha uwezo mkubwa na kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi huo uliowafanya waendelee kuifukuza kwa karibu Simba inayoongoza ligi.
Timu hizo zimepishana kwa pointi mbili huku Simba ikiongoza kwa pointi 38 baada ya timu zote kucheza michezo 16.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI



Post A Comment: