ads

UONGOZI wa Simba umesema wachezaji wake Waghana kipa Daniel Agyei na kiungo James Kotei wana vibali vya kufanya kazi ndio maana waliwacheza mchezo dhidi ya Ndanda FC mwishoni mwa wiki iliyopita.


Akizungumza  jana, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amewataka mashabiki na wapenzi wa Simba kupuuza habari zinazodai kwamba watapokwa pointi kwa kuwatumia wachezaji hao wakiwa hawana vibali vya kufanya kazi.

“Ndanda wasifikiri Simba inaongozwa na watu wasiojua taratibu hadi tuwachezeshe wachezaji bila vibali, acha wapeleke rufaa yao Bodi ya Ligi, watapewa majibu huko,” alisema Manara.

Ndanda FC imekata rufaa Bodi ya Ligi ikipinga Simba kuwachezesha wachezaji hao katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara ambapo Simba ilishinda mabao 2-0.

Akizungumzia sakata hilo jana, Katibu wa Ndanda, Suleiman Kachele alisema wana uhakika kwamba wachezaji hao walichezeshwa pasi na vibali vya kufanya kazi.

“Sisi tumekata rufaa kwa kuwa Simba iliwachezesha wachezaji ambao hawakuwa na vibali na sasa tunasubiri matokeo na matarajio yetu haki itatendeka tutapewa pointi tatu,” alisema Kachele.

Akifafanua suala la kikanuni kwa mchezaji aliyecheza mechi bila kibali cha kufanya kazi, Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Hamad Yahaya alisema:

“Kanuni zinasema kama mchezaji wa kigeni atacheza bila kibali cha kufanya kazi ataadhibiwa kwa kufungiwa, lakini sio timu kupokwa pointi”.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: