ads

MBUNGE wa zamani wa Kikwajuni, Parmuk Sing Hogani, amesema haikuwa mwafaka Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole,


Kuendelea kutetea msimamo wake wa muungano wa serikali tatu kwani kwa sasa ni sehemu ya kiongozi wa chama hicho chenye msimamo wa muundo wa serikali mbili.

Akizungumza  mjini hapa jana, Hogani alisema sera ya CCM ni muundo wa Muungano wa serikali mbili kuelekea moja, hivyo si mwafaka kwa Polepole kuendele na msimamo wake wa serikali tatu kwa kile alichoeleza unakwenda kinyume cha sera za chama chake.

“Kwa kuwa sasa ni kiongozi wa chama hatakiwi kuendelea kutetea hadharani msimamo wake wakati akifahamu unakwenda kinyume cha sera ya chama," alisema.

Hogani alisema CCM kwa kauli moja inapinga muundo wa Muungano wa serikali tatu kama ilivyokuwa imependekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa maslahi ya taifa, kulinda uhai wa Muungano wenyewe na mashikamano wa wananchi.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: