ads

RAIS wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, amevitaka vyuo vikuu vya Zanzibar kuisaidia Tume ya Kiswahili ya Afrika Mashariki kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya mawasiliano katika nchi wanachama wa jumuiya hiyo na kimataifa.


Dk. Shein alitoa wito huo alipokua akizungumza kwenye mahafali ya 16 ya Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Abdurahman Al-Sumait kilichopo Chukwani, mkoa wa Mjini Magharibi Unguja mwishoni mwa wiki.

Alivitaka vyuo vikuu hivyo kufanya tafiti katika nyanja mbalimbali za kiswahili na kutoa walimu wenye sifa ili kuendeleza lugha hiyo miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na duniani.

“Ni muhimu kwa vyuo vikuu vyetu kuhakikisha mitaala yao inazingatia mahitaji ya Tume ya Kiswahili ya Afrika Mashariki kwa sasa na baadaye,” alisema Dk. Shein katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mahmoud Thabit Kombo.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: