ads

HALI ya afya ya Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Vunjo, James Mbatia aliyefanyiwa operesheni ya mguu nchini India inaendelea vizuri na yupo nyumbani kwake Dar es Salaam akiendelea na matibabu.


Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Juju Danda, Mbatia kwa sasa yupo nyumbani kwake Mbezi Beach akiendelea kujiuguza.

“Unajua kwa kuwa amefanyiwa operesheni, itachukua muda kurejea katika hali yake ya kawaida, ila anaendelea vizuri kwa kweli na afya yake inazidi kuimarika,” alisisitiza Danda.

Mbatia alifanyiwa operesheni ya mguu Novemba 14, mwaka huu katika hospitali ya Zydus, India ambako alilazwa kuanzia Novemba 11 mwaka huu baada ya kusumbuliwa na maradhi ya mguu.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: