ads

MASHAHIDI wawili waliwasilisha ushahidi wao wakati kesi ya tuhuma za unyang’anyi wa kutumia silaha, inayomkabili Salum Njwete (34), maarufu ‘Scorpion’, iliponguruma kwenye Mahakama ya Ilala jijini Dar es Salaam jana.


Kesi hiyo ambayo ‘Scorpion’ anadaiwa kumtoboa macho Said Ally, mkazi wa Tabata jijini, ilianza majira ya saa 3:45 asubuhi hadi saa 5:10 mchana kwa shahidi wa pili na wa tatu kuwasilisha ushahidi wao. Shahidi wa kwanza ni Ally ambaye aliwasilisha ushahidi wake Desemba 14, mwaka huu.

Mashahidi wawili waliowasilisha ushahidi jana ni Stara Sudi, mke wa Ally na Yahaya Kisukari (23), mdogo wake na Ally.

Katika kesi hiyo inayosikilizwa na Hakimu Flora Haule, Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga na Wakili wa mshtakiwa, Juma Nassoro, waliwauliza maswali mashahidi hao kwa nyakati tofauti huku kitendo cha shahidi wa tatu (Kisukari) kudai kutopafahamu Buguruni kukionekana kumshtua Wakili Nassoro ambaye alimuuliza shahidi mara tatu kuhusu kulifahamu au kutolifahamu eneo hilo.

Shahidi huyo alidai hapajui Buguruni na hajawahi kufika katika eneo hilo na endapo akipelekwa na mtu yoyote, atalazimika kushikwa mkono ili asipotee ingawa kwa miaka minne anaishi eneo la Tabata lililopo jirani na Buguruni.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: