BEKI wa Yanga, Hassan Kessy, amesema
ataendelea kupambana na kuonyesha uwezo wake mazoezini ili kumshawishi
kocha Mzambia George Lwandamina kumpa nafasi kikosi cha kwanza cha timu
hiyo.
Kessy
amejikuta akipoteza namba kikosi cha kwanza kufuatia kurejea kwa Juma
Abdul ambaye kwa sasa anatumiwa na kocha huyo kwenye mechi za ligi.
Akizungumza juzi, Kessy alisema kugombea namba kwenye timu ni jambo la kawaida na ni jukumu lake kumshawishi kocha wake ampange.
"Hakuna timu ambayo inakosa ushindani wa namba na jambo hilo ni zuri kwa sababu linaongeza hali ya kujituma, naamini nitapata nafasi ya kucheza tu," alisema Kessy.
Alisema anachokifanya sasa ni kujituma zaidi mazoezini na kufanya kile ambacho kocha wake anamwelekeza.
Kessy alikuwa kikosi cha kwanza wakati Abdul alipokuwa nje ya uwanja akiuguza majeraha na tangu aliporejea na kuonekana kuwa fiti amekuwa chaguo la kwanza kwenye mechi za mzunguko wa pili zilizopita.
Akizungumza juzi, Kessy alisema kugombea namba kwenye timu ni jambo la kawaida na ni jukumu lake kumshawishi kocha wake ampange.
"Hakuna timu ambayo inakosa ushindani wa namba na jambo hilo ni zuri kwa sababu linaongeza hali ya kujituma, naamini nitapata nafasi ya kucheza tu," alisema Kessy.
Alisema anachokifanya sasa ni kujituma zaidi mazoezini na kufanya kile ambacho kocha wake anamwelekeza.
Kessy alikuwa kikosi cha kwanza wakati Abdul alipokuwa nje ya uwanja akiuguza majeraha na tangu aliporejea na kuonekana kuwa fiti amekuwa chaguo la kwanza kwenye mechi za mzunguko wa pili zilizopita.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI



Post A Comment: