ads

KANISA Katoliki Jimbo la Morogoro ,limeipongeza Serikali ya Rais Dk John Magufuli, kwa hatua inazoendelea kuchukua za uwajibikaji watumishi wa umma , kujenga nidhamu na kuboresha huduma mbalimbali za kiuchumi na kijamii.


Akizungumza jana baada ya kumaliza kuendesha misa takatifu ya sikukuu ya Krisimasi nje ya Kanisa kuu la Mtakatifu Patrice la Jimbo la Morogoro, Askofu Telesphor Mkude alisema kipindi cha mwaka mmoja tangu Serikali ya awamu ya tano iingie madarakani imeanza vizuri kwa kusimamia nidhamu na uwajibikaji kwa watumishi wa umma.

Pia alisema, imesimamia vyema uboreshaji wa huduma za kijamii zikiwemo za afya, miundombinu ya barabara na elimu ambazo ndani ya kipindi hicho zinakwenda vizuri.

Aliongeza kuwa , Rais Magufuli ameonesha ujasiri kubwa katika kusimamia uwajibikaji na nidhamu kwa watumishi wa umma ndani ya Serikali. Hatua hiyo ni pamoja na kuona matumizi ya fedha za umma zinazotokana na kodi za wananchi zinatumika katika kuhudumia huduma bora za kijamii kwa Watanzania.

" Kila awamu inaanza namna yake, kwa mwaka mmoja wa serikali ya awamu ya tano nadhani tunakwenda vizuri , huduma zinaonekana na zinapatikana vizuri."

Hivyo alisema miongoni mwa ujasiri uliochukuliwa na Rais Dk Magufuli katika serikali yake ni kulishughulikia suala la wafanyakazi wengi hewa walikuwepo tangu awamu zilizomtangulia ambapo mabilioni ya fedha yameokolewa na fedha hizo kuelekezwa katika huduma za jamii.

Askofu Mkude pia aliipongeza Serikali kwa kushughulikia na kuokoa mabilioni mengine ya fedha zilikuwa zikitolewa na kulipwa wanafunzi hewa kuanzia wa shule ya msingi hadi Vyuo Vikuu ambapo fedha hizo sasa zimeelekezwa kuboresha huduma za jamii.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: