ads

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imemuona Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima anayekabiliwa na kesi ya kushindwa kuhifadhi silaha, ana kesi ya kujibu.


Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Cyprian Mkeha alitoa uamuzi huo jana baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi wa upande wa Jamhuri pamoja na vielelezo.

Alisema kutokana na ushahidi huo, ameona upande wa Jamhuri umejenga kesi hivyo Gwajima na wenzake watatu, wana haki ya kujitetea, kuita mashahidi au kukaa kimya.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala alidai kuwa washtakiwa watajitetea kwa njia ya kiapo na watakuwa na mashahidi watatu.

Hakimu Mkeha alisema Desemba 13, mwaka huu, washtakiwa watajitetea na siku hiyo atasikiliza utetezi wa washtakiwa wote wanne pamoja na mashahidi wao.

Mbali na Gwajima, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni msaidizi wa askofu huyo, Yekonia Bihagaze (39), mfanyabiashara George Mnzava (43) na mkazi wa Kimara Baruti, Geoffrey Milulu (31).

Inadaiwa kuwa, Machi 29 mwaka jana, katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni A, washitakiwa walikutwa wakimiliki bastola aina ya Baretta yenye namba CAT 8802 bila kuwa na kibali kutoka mamlaka inayohusika na silaha na milipuko.

Aidha, inadaiwa washtakiwa hao walikuwa wakimiliki isivyo halali risasi tatu za bastola pamoja na risasi 17 za bunduki aina ya shotgun. Gwajima anadaiwa kushindwa kuhifadhi silaha katika hali ya usalama.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: