ads

RAIS wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, amezipongeza Serikali ya Oman na Cuba kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuendeleza miradi ya maendeleo sambamba na kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizo.


Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati alipokutana na mabalozi wa nchi hizo Ikulu mjini Unguja jana, Dk. Shein alizipongeza nchi hizo kwa kuendeleza uhusiano na ushirikiano wa kihistoria ambao umekuwa chachu katika kuimarisha juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kujileta maendeleo.

Akizungumza na Balozi wa Cuba anayemaliza muda wake wa kazi hapa nchini, Jorge Tormo, walisisitiza haja ya kuendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya pande mbili hizo.

Balozi Tormo alimuhakikikishia Dk. Shein kuwa Cuba inathamini sana uhusiano na ushirikiano wa kihistoria kati yake na Zanzibar na kuahidi kuendelea kuudumisha.

Alisema miradi yote ya maendeleo inayoishirikisha nchi yake itaendelezwa kwa juhudi kubwa, huku akimweleza Dk. Shein kuwa nchi yake itafarajika kwa kuwapo ushirikiano katika sekta ya utalii.

Mapema, Dk. Shein alifanya mazungumzo na Balozi mdogo mpya wa Oman, Ahmed bin Humoud Al Habsi, na kutumia fursa hiyo kuipongeza nchi hiyo kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika harakati zake za kukuza uchumi na kuimarisha maendeleo.

Kwa upande wake, Balozi Al Habsi aliyechukua nafasi ya Balozi Ali Abdulla Al Rashdi aliyemaliza muda wake wa kazi, alieleza kuwa Oman itaendeleza uhusiano na ushirikiano wake na Zanzibar na kupongeza hatua za maendeleo zilizofikiwa hapa nchini.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: