SIKU chache baada ya Umoja wa Mataifa (UN) kupiga kura kulaani ujenzi wa makazi ya walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi na Yerusalem Mashariki, Rais mteule wa Marekani, Donald Trump, amehoji ufanisi wa chombo hicho, akisema ni ‘genge la watu wakusanyikao na kupiga soga’.


Alitoa kauli hiyo baada ya jaribio lake la kutaka kupinga azimio lililokemea mpango wa Israel kuendelea kujenga makazi katika ardhi ya Wapalestina kushindikana.

Baraza la Usalama la UN (UNSC) limesema Israel inakiuka sheria za kimataifa kwa kujenga katika ardhi ya Wapelestina.

Azimio hilo lilipitishwa Ijumaa iliyopita, huku Trump akitoa onyo kuwa mambo yatakuwa tofauti wakati atakaposhika rasmi hatamu za uongozi wa Marekani.

Uamuzi wa utawala wa Rais Barack Obama kujiweka kando wakati UNSC ilipopiga kura hiyo ilihali ina kura ya turufu yenye uwezo wa kuitetea Israel, umekosolewa na Trump na kulaaniwa vikali na Israel.

Awali Desemba mwaka jana, Trump aliwahi kukaririwa akisema angependa kutoegemea upande wowote katika masuala ya Israel na Palestina.

Lakini msimamo wake ukawa ukibadilika kadiri kampeni za urais zilipoendelea akiegemea Israel zaidi.

Licha ya shutuma za Trump kwa UN, chombo hicho kwa miaka mingi kinashutumiwa na baadhi ya Serikali za magharibi kukosa ufanisi, huku mataifa yanayoendelea yakisema kinaburuzwa na mataifa tajiri.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: