
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
SIKU chache baada ya Umoja wa Mataifa (UN) kupiga kura kulaani ujenzi
wa makazi ya walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi na
Yerusalem Mashariki, Rais mteule wa Marekani, Donald Trump, amehoji
ufanisi wa chombo hicho, akisema ni ‘genge la watu wakusanyikao na
kupiga soga’.
Alitoa kauli hiyo baada ya jaribio lake la kutaka kupinga azimio
lililokemea mpango wa Israel kuendelea kujenga makazi katika ardhi ya
Wapalestina kushindikana.
Baraza la Usalama la UN (UNSC) limesema Israel inakiuka sheria za kimataifa kwa kujenga katika ardhi ya Wapelestina.
Azimio hilo lilipitishwa Ijumaa iliyopita, huku Trump akitoa onyo
kuwa mambo yatakuwa tofauti wakati atakaposhika rasmi hatamu za uongozi
wa Marekani.
Uamuzi wa utawala wa Rais Barack Obama kujiweka kando wakati UNSC
ilipopiga kura hiyo ilihali ina kura ya turufu yenye uwezo wa kuitetea
Israel, umekosolewa na Trump na kulaaniwa vikali na Israel.
Awali Desemba mwaka jana, Trump aliwahi kukaririwa akisema angependa
kutoegemea upande wowote katika masuala ya Israel na Palestina.
Lakini msimamo wake ukawa ukibadilika kadiri kampeni za urais zilipoendelea akiegemea Israel zaidi.
Licha ya shutuma za Trump kwa UN, chombo hicho kwa miaka mingi
kinashutumiwa na baadhi ya Serikali za magharibi kukosa ufanisi, huku
mataifa yanayoendelea yakisema kinaburuzwa na mataifa tajiri.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: