ads

Waziri wa muda mrefu na mbunge wa zamani wa Bunda, Steven Wasira amewajibu wanaodai kwamba amelazimika kustaafu siasa baada ya mpinzani wake, Ester Bulaya kuwashinda wapigakura wanne waliokuwa wakipinga ushindi wake wa ubunge wa Bunda Mjini na kusema hajastaafu na uzee haumzuii mtu kudai haki yake.


Juzi, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilimpa ushindi Bulaya katika kesi ya uchaguzi hali iliyotafsiriwa na wadadisi wa kisiasa kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa kisiasa wa Wasira.

Lakini jana, Wasira alipopigiwa simu na waandishi wetu kuelezea hatima yake ya kisiasa baada ya kesi hiyo, alisema wanaodai kuwa anatakiwa kustaafu siasa kwa sababu ni mzee hawana budi kuangalia kauli zao kwa sababu wapo wazee wengi anaowafahamu kwa majina na bado wapo madarakani.

“Suala la kusema nimestaafu siasa silijui na sijawahi kusema. Kesi hiyo inahusiana nini na siasa? Wapigakura wameona kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki. Hakuna uhusiano na uhusiano uliopo ni kwa sababu mimi ni shahidi na mimi niligombea,” alisema na kuongeza:

“Nataka wanipe ‘definition’ (maana) ya kustaafu siasa. Je, ni kunyamaza, nisitoe maoni. Mbona wapo watu walikuwa wanasiasa na bado wanatoa maoni ya kisiasa tena yenye manufaa makubwa?”

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: