ads

Nyota Cristiano Ronaldo amerudi kwa kasi akifumania nyavu kwa kishindo, baada ya kufunga mabao matatu (hat trick) na kuiwezesha Real Madrid kuilaza Atletico Madrid kwa 3-0 katika uwanja wa Vicente Calderon kuamkia leo.


Kwa mantiki hiyo, Madrid imejiimarisha kileleni kwa tofauti ya pointi nne dhidi ya mahasimu wao Barcelona, ambayo awali ililazimishwa sare ya bila kufungana na Malaga.

Zikiwa zimecheza michezo sawa, Real Madrid inaongoza baada ya kujikusanyia pointi 30, ikifuatiwa na Barcelona yenye alama 26 huku Atletico Madrid ikisalia na pointi 24.

Ronaldo alianza kutikisa nyavu katika dakika ya 23 baada ya kupiga mkwaju wa adhabu na kuwababatiza mabeki wa Atletico. Alizidi kuwapa furaha mashabiki wa Madrid baada ya kufunga kwa njia ya penalti dakika ya 71 kabla ya kukamilisha hat-trick katika dakika ya 77, baada ya kuunganisha krosi safi iliyopigwa na winga mwenye mbio, Gareth Bale.
 
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: