ads

Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe amesema anaamini Edward Lowassa hakuenguliwa kwa haki na CCM katika mchakato wa kumpata mgombea urais wa chama hicho, na kwamba waziri mkuu huyo wa zamani si pekee ambaye amekumbana na uonevu kama huo.


Bashe, ambaye ameingia bungeni kwa mara ya kwanza katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana akipeperusha bendera ya CCM, pia amesema kashfa zote zinazoikumba Serikali hutengenezewa suluhisho kwa malengo fulani na si kutafuta muafaka wa haki.

Kiongozi huyo wa zamani wa Umoja wa Vijana wa CCM alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi.

Bashe, ambaye alikuwa kambi ya Lowassa wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM, alisema ingawa hana uhusiano tena wa kisiasa na kada huyo, anaona tukio lake kuwa ni historia ya kutotendea haki wanachama wengi wa CCM. “Si Lowassa pekee, wako wengi,” alisema Bashe katika mahojiano hayo.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: