ads

Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) kimewaomba wawekezaji kutoka nchini China kuja kuwekeza viwanda vyao hapa nchini hususani vile vinavyotumia teknolojia rahisi na vinavyoajiri idadi kubwa ya watu katika uzalishaji.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Clifford Tandari ametoa wito huo leo Jijini Dar es Salaam katika mkutano ambao Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imekutana na wafanyabiashara zaidi ya 200 kutoka nchini China wanaofanya biashara zao hapa nchini.

Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipakodi wa TRA Bw. Richard Kayombo amesema hii ni mara ya kumi na sita TRA inakutana na wafanyabiashara hao kutoka nchini China kwa lengo la kuwawezesha kufahamu mifumo ya kodi nchini.

Huduma za uwekezaji zinaenda sambamba na ushauri wa kisheria hususani zile zinazohusiana na masuala ya kodi kwa wageni kama anavyoeleza mwakilishi wa kampuni ya uwakili ya ABC Attorneys Bw. Sunday Godfrey.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: