![ads](http://1.bp.blogspot.com/-J5aEnGVep5k/WJTrf2fzuPI/AAAAAAAAU5U/_iuE-DY1RHAM5_hqPHb-UuNbabG2xn2nwCK4B/s1600/AdvertiseHere.jpg)
Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) kimewaomba wawekezaji kutoka nchini
China kuja kuwekeza viwanda vyao hapa nchini hususani vile vinavyotumia
teknolojia rahisi na vinavyoajiri idadi kubwa ya watu katika uzalishaji.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Clifford Tandari ametoa wito huo leo
Jijini Dar es Salaam katika mkutano ambao Mamlaka ya Mapato nchini (TRA)
imekutana na wafanyabiashara zaidi ya 200 kutoka nchini China
wanaofanya biashara zao hapa nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipakodi wa TRA Bw. Richard Kayombo amesema hii ni mara ya kumi na sita TRA inakutana na wafanyabiashara hao kutoka nchini China kwa lengo la kuwawezesha kufahamu mifumo ya kodi nchini.
Huduma za uwekezaji zinaenda sambamba na ushauri wa kisheria hususani zile zinazohusiana na masuala ya kodi kwa wageni kama anavyoeleza mwakilishi wa kampuni ya uwakili ya ABC Attorneys Bw. Sunday Godfrey.
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipakodi wa TRA Bw. Richard Kayombo amesema hii ni mara ya kumi na sita TRA inakutana na wafanyabiashara hao kutoka nchini China kwa lengo la kuwawezesha kufahamu mifumo ya kodi nchini.
Huduma za uwekezaji zinaenda sambamba na ushauri wa kisheria hususani zile zinazohusiana na masuala ya kodi kwa wageni kama anavyoeleza mwakilishi wa kampuni ya uwakili ya ABC Attorneys Bw. Sunday Godfrey.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: