ads

Umoja wa Ulaya(EU) umeishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupendekeza kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.


Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini, Van de Geer amesema kuwa anategemea mkwamo wa kisiasa kati Serikali ya Zanzibar na Chama Kikuu cha Upinzani Visiwani humo CUF kutatuliwa siku za karibuni.

Balozi de Geer amesema kuwa Umoja wa Ulaya uko kwenye mazungumzo na Serikali ya Rais John Magufuli na Umoja huo unategemea Rais Magufuli ataanzisha majadiliano kutatua mgogoro uliopo na hatimaye CUF kuingizwa kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Serikali ya Umoja wa Kitaifa ilifikia tamati baada ya Uchaguzi wa Marudio, tarehe 20, Machi 2016 baada ya CUF kususia uchaguzi huo kwa madai kuwa wa Oktoba 25, 2015 uliofutwa walishinda na wa marudio ulikuwa hauko kisheria na usingekuwa huru na haki.

Umoja wa Ulaya umepunguza mahusiano yake na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Dkt. Ali Mohamed Shein tangu Ujumbe wa waangalizi wa Uchaguzi kutoka Umoja wa Ulaya uliokuwa ukiongozwa na Bi. Judith Sargentini kupinga Uchaguzi wa Marudio wa Machi 20, 2016.

Chama cha CUF ambacho kinaonekana kiko tayari kwa ajili ya mazungumzo, Serikali ya Zanzibar imewahi kukaririwa ikisema kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa(SUK) ilishazikwa, japokuwa inatambuliwa na Katiba ya Zanzibar.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: