MTUHUMIWA wa unyang'anyi wa kutumia silaha, Salum Njwete(34), maarufu kwa jina la ‘Scorpion’, jana aliishangaza Mahakama ya Wilaya ya Ilala, baada ya kutaka iendeshe kesi yake kwa kasi anayotaka yeye.

Akiwa kizimbani kama mtuhumiwa pekee, ‘Scorpion’ alitaka asomewe maelezo ya awali ya kesi yake japokuwa hakupewa nafasi ya kujieleza kwa lolote.

'Scorpion' aliomba asomewe maelezo ya awali sekunde chache baada ya Wakili wa Serikali, Chesensi Gavyole kuiambia mahakama kwamba upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Baada ya Gavyole kumaliza maelezo hayo, Hakimu Frola Haule anayesikiliza kesi hiyo alimwambia mtuhumiwa huyo kuwa ataanza kusomewa maelezo ya awali Novemba 30.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: