
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KLABU ya Simba imekubali kulipa dola za Marekani 120,000 (mabazo ni
zaidi ya Sh milioni 240 kwa klabu ya Sonderjiske ya Denmark ili
kumrejesha mshambuliaji wake wa zamani, Mganda Emmanuel Okwi.
Baada ya klabu hiyo kukamilisha kulipa kiasi hicho cha fedha,
mchezaji huyo atarejea kuichezea Simba kwa mkataba wa mwaka mmoja kwa
mujibu wa makubaliano hayo.
Simba ilimuuza Okwi kwa dola 100,000 mwaka juzi Denmark, lakini
kutokana na mchezaji huyo kutopata nafasi ya kucheza Ulaya, imeamua
kumrejesha na makubaliano yamefikiwa Sh milioni 240.
“Dola 120,000 tu wale jamaa wanataka watuachie Okwi. Na Okwi naye
atasaini kwa mshahara tu mkataba wa mwaka huu, hatumpi dau la kusaini
yeye,”kimesema chanzo kutoka Simba.
Taarifa za mitandao ya kujamii jana zilieleza kuwa, Okwi ni mchezaji
aliyeipa faida kubwa Simba ndani na nje ya uwanja wakati ule akiichezea
klabu hiyo ya Msimbazi.
Mbali na kuwasaidia Wekundu hao wa Msimbazi kushinda matajii
mbalimbali tangu ajiunge nao kwa mara ya kwanza mwaka 2010, mchezaji
huyo pia aliinufaisha kifedha Simba.
Simba ilimuuza Okwi Etoile du Sahel ya Tunisia Januari mwaka 2013 kwa
dau la rekodi kwa klabu za Tanzania, dola 300,000, ingawa baada ya muda
akaingia kwenye mgogoro na klabu hiyo ya Tunisia.
Mtafaruku ulianza
baada ya Okwi kuchelewa kurejea mjini Sousse mkoani Sahel baada ya
ruhusa ya kwenda kuichezea timu yake ya taifa, Uganda.
Okwi naye akadai Etoile walikuwa hawamlipi mishahara na kufungua kesi
FIFA, ambayo mwisho wa siku alishinda kwa kuruhusiwa kutafuta timu
nyingine ya kuchezea kulinda kipaji chake, wakati wa mgogoro wake na
klabu ya Tunisia.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: