ads

Profesa Ibrahim Lipumba Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) aliyefutwa uanachama na Baraza Kuu la Uongozi Taifa la Chama hicho, amesema usaliti uliofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wake Dkt. Wilbroad Slaa na kukiuka makubaliano ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika kipindi cha kampenzi za uchaguzi mkuu wa 2015 utakigharimu chama hicho.


Lipumba ameyasema hayo Novemba 26, 2016 katika mkutano wake na baadhi ya viongozi wa kata za Jimbo la Temeke kwenye Ukumbi wa Sunrise ulioko Tandika jijini Dar es Salaam.

“Usaliti wa Chadema kwa Dkt. Slaa utaendelea kuigharimu na ndio maana hawataki nirudi katika wadhifa wangu na nikirudi watakwisha,” amesema.

Amedai kuwa, usaliti wa Chadema umesababisha upinzani kupokonywa ajenda yake ya ufisadi na kuruhusu Rais John Magufuli kuitumia ajenda hiyo kumaliza nguvu ya upinzani.

“Rais Magufuli ametunyang’anya ajenda ya kusimamia ufisadi, leo hii Chadema hawana ajenda ya kupinga ufisadi kwa sababu ya kumuasi Slaa,” amesema.

Kuhusu Ukawa Lipumba amedai kuwa, baadhi ya viongozi wa Chadema wanautumia umoja huo kuiua CUF Bara huku akituhumu baadhi ya viongozi wa CUF kuwa wananjama za kukiuza chama hicho.

“Viongozi wanajua dhahiri athari za Ukawa na hata Julias Mtatiro alipokuwa anagombea Ubunge Segerea alinitumia sms na sijaifuta ipo, akisema kuwa kuna athari zitakazotukuta kuhusu mpango wa Chadema wa kusimamisha wagombea katika majimbo ya CUF, leo hii anaungana nao,” amesema.

Aidha, amesema alifikia hatua ya kujiudhuru mwezi Agosti mwaka jana uenyekiti wa CUF kwa madai ya kutokubaliana na hali ya kuwa mpiga debe wa Edward Lowassa aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya Chadema na mwamvuli wa Ukawa.

“Nilikataa kuwa mpigadebe wa Lowassa, niligombea urais mara nne leo hii nisimame kumpigia debe Lowassa? Ambaye kwenye orodha ya majina ya mafisadi jina lake lilikuwa namba nmoja. Nisingeweza fanya hivyo nikaona bora kujiudhuru,” amesema.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: