ads

KOCHA Mkuu wa Simba, Joseph Omog, ameshtukia safu ya benchi la ufundi la mahasimu wao, Yanga ikiwepo kuanza mapema maandalizi yao kwa ajili ya mzunguko wa pili na kuwataka wachezaji wake wote kufika kwa wakati siku ambayo wamepanga kuanza mazoezi ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.


Juzi Ijumaa Yanga, ilitangaza benchi jipya la Ufundi ambalo litakuwa chini ya kocha Mzambia George Lwandamina huku aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Mholanzi Hans Pluijm akipandishwa cheo na kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu hiyo.

Akizungumza  hivi karibuni Omog, alikiri kuwa mikakati ya wapinzani wao Yanga imemtia hofu na kutoa mwito kwa wachezaji wake popote walipo kufika kwa wakati ili kuanza maandalizi yao ya mzunguko wa pili wakiwa wote na kupeana mbinu mbadala, ambazo zitaweza kuwasaidia kuwapa ubingwa msimu huu.

“Lazima nikiri kuwa Yanga ndiyo timu ambayo inanipa presha kwa sababu tunatofautiana nao kwa pointi mbili, lakini kitendo cha kubadilisha benchi lao la ufundi nacho kinaonesha namna walivyokuwa makini katika kuendelea kuwa tena mabingwa msimu huu kutokana na ubora wa kocha na Mkurugenzi wa ufundi,” alisema Omog.

Kocha huyo alisema ingawa hafahamiani vizuri na Lwandamina, lakini anaonesha ni kocha mwenye uwezo mkubwa, kutokana na mafanikio aliyoipa Zesco United, sawa na Pluijm ambaye amepewa cheo cha Ukurugenzi hivyo anaamini Yanga ya mzunguko wa pili itawasumbua zaidi kutokana na uwepo wao.

Alisema anataka kuanza maandalizi mapema, lengo likiwa ni kurudisha umoja na ufiti wa wachezaji wake pamoja na kuwajenga kisaikolojia kwa sababu watakuwa wakicheza kwa presha kutokana na tofauti ya pointi mbili kati yao na mahasimu wao Yanga.

“Tutacheza kwa presha kubwa kwa sababu ya tofauti ya pointi mbili hofu yetu ni kuhofia kupoteza mchezo kwamba wapinzani wetu watatupita na kibaya zaidi tuna mechi nyingi za ugenini mzunguko wa pili", alisema na kuongeza:

“Endapo tutaanza maandalizi kwa pamoja niwazi tutaweza kurudisha ari ya waliyokuwa nayo wachezaji wetu na kuweza kupambana na Yanga kwenye mbio za ubingwa,” alisema Omog.

Simba imepoteza michezo miwili sawa na Yanga kwenye mzunguko wa kwanza na tofauti yao ni pointi mbili na kocha Omog, amepania timu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu na ndiyo maana amewasisitiza wachezaji wake kujitokeza kwa wingi siku ya kwanza ya mazoezi ya timu hiyo.

Wakati huo huo, Omog amewataka viongozi wa klabu hiyo kusajili wachezaji watatu tu, ambao ni kipa, beki na mshambuliaji.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: