ads

WAHITIMU, viongozi na wageni waliohudhuria Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) mkoani Morogoro, waliingiwa na simanzi wakati mtoto, Tamar Aaron Mbogho (11), alipojitokeza na kupokea Shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD), akimwakilisha mama yake Swai Sophia Faustin ambaye alifariki dunia miezi sita kabla ya kufika siku ya mahafali.


Tamar, mtoto pekee wa marehemu, ambaye baba yake mzazi ni Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro, Aaron Mbogho alifika katika hafla hiyo akiwa ameambatana na ndugu zake kadhaa, tayari kwa ajili ya kupokea heshima hiyo kwa niaba ya mama yake.

 Kwa mujibu wa Mbogho, mkewe Dk Sophia alifariki dunia Mei 21, 2016, wakati huo akiwa ameshahitimu masomo yake kikamilifu na alisema Tamar ni mtoto wa pekee wa Sophia.

"Alikuwa ni mmoja wa wahitimu waliopaswa kutunukiwa shahada hiyo kwa sababu tayari alishahitimu na kubakia muda wa mahafali, lakini bahati mbaya akafariki dunia kabla ya muda kuwadia,” alisema na kuongeza.

"Binti yetu alipenda kwenda kuchukua shahada ya mama yake na alisindikizwa na ndugu zake wa familia. Ameniambia malengo yake ni kusoma kwa bidii ili aweze kupata Shahada ya Udaktari wa Falsafa kama mama yake, " alisema Mbogho.

Katika mahafali hayo yaliyofanyika juzi katika Kampasi ya Solomon Mahlangu, Mazimbu, wahitimu 61 walifuzu na kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Falsafa ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.

Naibu Makamu Mkuu Taaluma wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Peter Gilla, alisoma orodha ya watunukiwa ambapo pia alitaja jina la mwanafunzi asiyekuwapo ambaye alifariki dunia, lakini akiwa amefuzu na anastahili kupata Shahada ya PhD ya Chuo Kikuu hicho ambaye ni Sophia.

Hivyo, Mwenyekiti wa Mahafali hayo, Dk Benno Mrembuka, alimwongoza mtoto Tamar kwenda kupokea shahada hiyo kutoka kwa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Fedha na Utawala, Profesa Yonika Ngaga, hali iliyoleta simanzi na huzuni kwa washiriki waliokuwepo katika mahafali hiyo.

Baadaye Tamar alielekezwa kufika mbele ya meza kuu ili kuwapa mkono wageni mbalimbali ambao walitumia nafasi hiyo kumfariji kutokana na kumpoteza mama yake mzazi ambaye alikuwa ni mhitimu.

Katika hatua nyingine, Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Gerald Monela, alisema SUA imeendelea kutoa wahitimu wa Shahada ya Sayansi na Ualimu katika masomo ya sayansi kwa ajili ya kukidhi mahitaji makubwa ya walimu wa kufundisha shule za sekondari nchini.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: