ads

KOCHA Mkuu mpya wa Yanga, George Lwandamina amekanusha taarifa za kuleta wachezaji kutoka Zesco lakini pia amekiri wachezaji wa Tanzania ni legelege ukilinganisha na wale wa Zambia.


Lwandamina aliyasema hayo jana wakati akitambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari pamoja na Mkurugenzi wa Ufundi wa Yanga, Hans Pluijm.

Lwandamina alisema hana mpango wa kubadilisha chochote kwenye benchi la ufundi pamoja na wachezaji huku akikanusha kuwaleta nchini wachezaji Jesse Were na Misheck Chaila, lakini akasema amekabidhiwa jukumu zito ila analichukulia kama changamoto kuhakikisha Yanga inafanya vema.

“Nitapambana kuhakikisha Yanga inafanya vizuri, najua ni changamoto mpya kwangu, lakini nitafanya kila linalowezekana kuhakikisha tunafanya vizuri kuanzia kwenye ligi ya nyumbani hadi klabu Bingwa Afrika,” alisema Lwandamina.

"Nasikia tetesi kuhusu wachezaji wapya kutoka Zesco kusajiliwa Yanga, naomba ifahamike kuwa kama kocha mkuu sijui chochote labda mchakato huo unafanyika bila mimi kushirikishwa, kwani kikosi kilichopo ndicho nitaendelea nacho," alisema Lwandamina.

Pia Lwandamina alisema hakuna wachezaji aliowaleta japo amekiri wachezaji wa Tanzania hawako fiziki kama wa Zambia kwani alishawaona wakati wakicheza na Ruvu Shooting kwenye mechi ya mwisho ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Akimzungumzia mtangulizi wake, Lwandamina amemsifu Pluijm kwa kusema amefanya kazi nzuri na kuahidi kufuata nyayo zake kwa kushirikiana naye bega kwa bega kuhakikisha Yanga inapata mafanikio zaidi.

Mkurugenzi mpya wa ufundi, Pluijm alisema yeye hana shida na kubadilishiwa majukumu kikubwa ataendelea kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa mkataba wake. Pluijm alianza kuifundisha Yanga 2014 na ameiongoza katika mechi 128 kwenye awamu mbili, akishinda 80, sare 25 na kufungwa 23.

Katika mechi 19 za nusu msimu mwaka 2014, alishinda 11, sare sita na kufungwa mbili, wakati katika mechi 110 za tangu mwaka jana, alishinda 69, sare 19 na kufungwa 21.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: