ads

ASKARI wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), Nassir Hassan Jecha, amefukuzwa kazi kwa tuhuma za kumfanyia mwanafunzi mtihani wa kidato cha nne.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Nassor Ali Hassan, alisema askari huyo alikamatwa katika chumba cha mtihani katika Shule ya Sekondari ya Mwanakwerekwe A, akifanya mtihani wa somo la Kiswahili kwa kutumia jina la Said Mwinyi Haji.

Alisema baada ya wasimamizi wa mtihani kumkamata askari huyo na kubaini kuwa si mtahiniwa halali, Jeshi la Polisi lilifanya uchunguzi na kubaini kuwa ni askari wao na alikuwa akimfanyia mtihani mtu mwengine.

“Jeshi la Polisi halipendi kuona linatiwa doa na kasoro kwa kuwa lina dhamana kubwa kwa taifa, hivyo tunapogunduwa kosa lolote lazima tufanye uchunguzi na likimhusisha askari wetu ni lazima kumchukulia hatua zinazostahili,”alisema.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: