
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
WAATHIRIKA wa Ukimwi wanakabiliwa na hatari ya kuugua
magonjwa yasiyoambukiza ya saratani na kupata matatizo ya misuli ya moyo,
kutokana na athari za matumizi ya Dawa za Kupunguza Makali ya Virusi vya Ukimwi
(ARV).
Utafiti mpya uliochapishwa juzi na Taasisi Utafiti wa
Saratani na Virusi Vinavyosababisha Ukimwi (VVU) ya Chuo Kikuu cha Califonia,
San Francisco (UCSF), umeeleza kuwa saratani hutokea katika tishu za mwili,
ambako virusi hivyo hukimbilia kujificha ili visifikiwe na ARV.
Taarifa ya Mtaalamu wa Maabara, Profesa Michael McGrath
wa UCSF iliyochapishwa katika jarida la
Virology la mwezi huu, imeeleza imependekeza
utafiti wa haraka ufanyike ili kutafuta muafaka wa tatizo hilo.
Wanasayansi hao wameelezwa kuwa walifanya utafiti huo
baada ya kubaini kuwa baadhi ya waathirika wa VVU wanaotumia ARV na kuwa na
afya nzuri, hujikuta wakifa ghafla.
“Baada ya kuchunguza tukabaini kuwa vifo hivi
vinasababishwa na saratani pamoja na matatizo ya misuli ya moyo,” alisema
Profesa McGrath.
Hali hiyo, anasema iliwafanya waendelee na utafiti ambao
matokeo yake wameyapata mwezi huu kwa kubaini kuwa virusi vinavyojiviche kwenye
tishu za mwili ambako havifikiwi na ARV ndivyo vinasababisha tatizo hilo.
Tangu dawa za ARV zianze kutumika zimeonekana kuzuia VVU
kuathiri seli nyeupe za binadamu maarufu kama CD4.
Matumizi hayo yameweza kuwafanya baadhi ya waathirika
kupima na kutoonekana tena kuwa na VVU kwenye mfumo wao wa damu lakini wakiacha
kutumia ARV huzuka ghafla na kuanza kuonekana vikishambulia CD4.
Profesa McGrath anasema kuwa katika utafiti wao wamebaini
kuwa kwenye tishu za mwili wa binadamu ambako VVU hujificha vinasababisha
tatizo la saratani na matatizo ya moyo.
“Hivi vifo vya wagonjwa walio katika matumizi ya ARV
vinaelekea vinatokana na uwapo wa virusi hawa waliojificha kwenye tishu baada
ya kushindikana kufikiwa na dawa ya kuwaangamiza,” alisema Profesa McGrath na
akifafanua:
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: