
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MWENYEKITI wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku amepongeza
ukaguzi wa vyeti pamoja na mfumo wa uchumi, unaofanywa na Serikali ya
Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli.
Alisema kuwa ni hatua nzuri ya kurejesha nidhamu na maendeleo ya nchi na kuwataka wananchi kumuunga mkono na sio kulalamika.
Butiku alisema hayo juzi kwenye mazungumzo maalumu na gazeti hili,
ambapo alisema kuwa kinachoendelea kwa sasa ni utekelezaji wa sheria na
kanuni ambazo awali zilichezewa.
Alisema kushindwa kufuatwa kwa taratibu kulitengeneza mianya
mbalimbali kwa wananchi kujiamulia mambo yao, huku wengine wakiichezea
elimu ambayo ndio msingi wa taifa.
Butiku alionesha kukerwa zaidi na utitiri wa vyeti vya kufoji,
uliokuwa umekithiri serikalini na kuipongeza serikali kwa uamuzi wake wa
kukabiliana na hali hiyo sasa, kwa kufanya uhakiki wa vyeti vya
watumishi wa umma.
Alisema kuwa inashangaza kuona kuwa kuna watu walikuwa wamefikia hadi
hatua ya kuwa na vyeti vya juu vya Shahada ya Uzamili (Masters) na
Uzamivu (PHD), lakini vya kidato cha nne hawana.
βKile kinachoendelea kwa sasa ni utekelezaji wa ahadi ya kurejesha
mifumo ya nidhamu kwenye serikali, sasa kinachotakiwa ni kuunga mkono
kwa kuhakikisha kuwa malengo ya Rais yanatimia kwa sasa,β alisema
Butiku.
Hivi Karibuni Butiku akizungumza na Gazeti Moja la kila Siku alinukuliwa akisema kuwa Chama Chake cha CCM kimekithiri kwa Rushwa hali aliyosema kuwa ni kinyume na miiko na matakwa ya katiba ya chama hiko.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: