ads
 
ALIYEKUWA Mbunge wa Kigoma Kusini na Mkuu wa Idara ya Habari na Uenezi wa Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila amesema amepatwa na mfadhaiko kwa kitendo cha kuahirishwa kwa mahojiano katika Kituo cha Televisheni cha Clouds kupitia kipindi cha 360.

Kafulila alisema amepatwa na mfadhaiko mkubwa kwa mahojiano hayo ambayo yalikuwa yanahusu kujadili mambo mbalimbali ya nchi na kwamba kitendo hicho kina mkono wa viongozi wa Serikali wakubwa.

“Inasikitisha kuona kipindi kimetangazwa tangu jana (juzi) na nimefika na kuvaa kipaza sauti halafu unaambiwa kuna agizo kutoka kwa mkurugenzi kipindi kisirushwe nimefadhaika sana sana,” alisema.

“Hadi kipindi cha magazeti saa mbili asubuhi nilikuwa studio na mtangazaji akatangaza kuwa  baada ya magazeti Kafulila ataingia kujadilia masuala mbalimbali yanayoendelea nchini.

Nikiwa studio tayari nimevaa kipaza sauti, ikaombwa radhi kwamba kuna maelekezo kutoka kwa mkurugenzi kuwa kipindi kisirushwe,” aliongeza

Kafulila alisema anadhani kulikuwa na maelekezo ya ziada nje ya mfumo wa Clouds Tv kwa sababu haamini kama tangazo limerushwa kutwa nzima jana (juzi) na jana asubuhi bila mkurugenzi huyo kujua.

Mbunge huyo wa zamani alihoji iwapo mkurugenzi huyo hakujua bado vipindi ni suala la wataalamu wa utangazaji kuliko mmiliki na kwamba hajajua hofu yao ilikuwa wapi.

Mkuu huyo wa idara alisema kinachoondelea kwa sasa kwa mtazamo wake ni kuminya uhuru wa vyombo vya habari, huku akibainisha kuwa Sheria ya habari inayokwenda kupitishwa bunge lijalo, vyombo vyote vitakuwa chini ya ulinzi wa dola.
 
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: