ads

Mchakato unaofanywa na klabu ya Yanga wa kutaka kukodisha nembo na timu hiyo kwa mwenyekiti wao, Yusuf Manji unakwenda kinyume na Katiba ya klabu hiyo kongwe nchini.


Katiba ya Yanga ya 2010 inayotambuliwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Baraza la Michezo Tanzania (BMT), ibara ya 56, ibara ya 56, ibara ya 56 inatambua suala la klabu hiyo kubadilika kuwa kampuni ya umma na siyo mali ya mtu mmoja au kikundi.

Ibara ya 56 yenye kichwa cha habari, Kampuni ya Umma ya Yanga inaonyesha jinsi klabu hiyo itakavyofuata utaratibu wa kubadilika na kuingia katika mfumo wa kampuni.

Ibara ya 56 (1), inaeleza kuwa kutakuwa na kampuni itakayojulikana kama Young Africans Corporation Limited itakayosajiliwa chini ya Sheria ya Makampuni ikiwa kampuni ya umma yenye hisa.

Ibara ya 56(2), “Wanachama wote ambao katika tarehe ya marekebisho ya katiba ya mwaka 2007 wako hai, watakuwa, kwa nguvu ya uanachama wao, wanahisa katika kampuni kwa kiwango cha idadi ya hisa watakazopata kwa mujibu wa mwafaka wa Yanga uliofikiwa Juni 6, 2006.

Ibara ya 56 (3) inasema, “Klabu itamiliki hisa zilizo sawa na asilimia hamsini na moja (51) ya hisa zote zilizopo katika kampuni.
Ibara ya 56 (4) inasema,” Mkutano mkuu wa uchaguzi utachagua wanachama wawili ambao siyo miongoni mwa viongozi wa klabu kuwa wajumbe wa bodi ya wakurungenzi wa kampuni kwa ajili ya kuwakilisha masilahi ya klabu kwenye kampuni.

Hivyo, uamuzi wa Manji kuanzisha kampuni, Yanga Yetu Limited anayoimiliki kwa asilimia 99 na kukodisha timu na nembo ya klabu hiyo kwa kipindi cha miaka kumi unapingana na Ibara 56 (3) inayotoa nafasi kwa klabu kumiliki asilimia 51 za hisa.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: