ads
 
BARAZA la Vijana la Chadema (Bavicha) limetaja moja ya sababu za wanafunzi wa elimu ya juu kukosa mikopo kuwa ni Serikali kushindwa kulipa deni la Sh60 Bilioni inayodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.

Mwenyekiti wa Bavicha, Protrobas Katambi, alisema kuwa baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakipiga simu na kueleza kuwa wengi wao wameshindwa kupata mikopo katika mwaka huu wa masomo.

Alitaja baadhi ya vyuo ambavyo wanafunzi wake walikuwa wakiipigia simu na kueleza tatizo hilo kuwa ni Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo Kikuu Huria (OUT), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), na vinginevyo.

Alisema kutokana na changamoto hiyo ni dhahiri kuwa kuna vyuo vipo hatarini kufungwa hivyo ni vyema serikali ikafanyia kazi ili wanafunzi hao wapewe mikopo na kuondokana na adha hiyo.

Alisema kutokana na changamoto hiyo Bavicha  limetoa siku saba na kumtaka Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako atoe ufafanuzi kuhusu suala hilo ili kuwezesha wanafunzi hao kupata mikopo na waweze kurudi vyuoni kuendelea na masomo yao.

“Hali ya elimu kwa wanafunzi wa elimu ya juu, vyuo vipo hatarini kufungwa hivyo tunamtaka Ndalichako aseme kuwa suala hilo litafanywaje ili wanafunzi hao waweze kupewa mikopo na kama atashindwa amwambie waziri mkuu atoe tamko na yeye akishindwa basi Rais apewe jukumu hilo,” alisema. 
 
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: