BARAZA la Vijana la Chadema (Bavicha)
limetaja moja ya sababu za wanafunzi wa elimu ya juu kukosa mikopo kuwa ni
Serikali kushindwa kulipa deni la Sh60 Bilioni inayodaiwa na Bodi ya Mikopo ya
Elimu ya Juu.
Mwenyekiti wa Bavicha, Protrobas Katambi,
alisema kuwa baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakipiga simu na kueleza kuwa wengi
wao wameshindwa kupata mikopo katika mwaka huu wa masomo.
Alitaja baadhi ya vyuo ambavyo wanafunzi
wake walikuwa wakiipigia simu na kueleza tatizo hilo kuwa ni Chuo Kikuu cha
Dodoma (UDOM), Chuo Kikuu Huria (OUT), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),
Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), na
vinginevyo.
Alisema kutokana na changamoto hiyo ni dhahiri
kuwa kuna vyuo vipo hatarini kufungwa hivyo ni vyema serikali ikafanyia kazi
ili wanafunzi hao wapewe mikopo na kuondokana na adha hiyo.
Alisema kutokana na changamoto hiyo
Bavicha limetoa siku saba na kumtaka
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako atoe
ufafanuzi kuhusu suala hilo ili kuwezesha wanafunzi hao kupata mikopo na waweze
kurudi vyuoni kuendelea na masomo yao.
“Hali ya elimu kwa wanafunzi wa elimu ya
juu, vyuo vipo hatarini kufungwa hivyo tunamtaka Ndalichako aseme kuwa suala
hilo litafanywaje ili wanafunzi hao waweze kupewa mikopo na kama atashindwa
amwambie waziri mkuu atoe tamko na yeye akishindwa basi Rais apewe jukumu
hilo,” alisema.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI



Post A Comment: