
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji, amesitisha
kuendelea na zoezi la kuikodisha timu na nembo ya klabu hiyo na
kuwaambia wasaidizi wake, wasitishe mipango yote ya maendeleo waliyokuwa
wameanza kuifanya.
Manji amewaambia wasaidizi wake kusitisha maandalizi ya Ligi ya
Vijana ya Matawi ya Yanga, lakini amewaambia waandae siku rasmi ambayo
atazungumza na vyombo vya habari na kuwaomba radhi Wanayanga ambao
wamemuunga mkono muda wote.
Habari za uhakika ambazo Championi Jumatano limezipata, zinasema
Manji alizungumza na wasaidizi wake jana mchana ikiwa ni dakika chache
baada ya TFF kufanya mkutano na waandishi wa habari na kusema hawatambui
suala la Yanga kuikodisha timu na nembo kwa Kampuni ya Yanga Yetu Ltd,
kwa miaka 10.
“Leo alionekana ni kama mtu aliyekata tamaa au asiyefurahishwa na jambo. Amewaita wasaidizi wake na wamefanya kikao, hakikuwa kirefu sana.
“Amewaambia ameamua kuachana na masuala ya kuikodisha Yanga, pia amesema ameona ni vizuri kuachana na masuala ya mpira.
“Kilichomuudhi ni wale wasiotaka mchakato wa mabadiliko Yanga, lakini hawatoi hoja za msingi,” kilieleza chanzo.
“Wasaidizi wake walikuwa wameanza mchakato wa kutengeneza mfumo wa Ligi ya Vijana ya Matawi ambao ungeigharimu Yanga yetu takribani Sh milioni 280 kwa ajili ya vifaa, uendeshaji na kadhalika.“Lakini kuna suala amelizungumzia la uchaguzi, hilo sijaelezwa vizuri. Huenda Yanga wakaitisha uchaguzi tena ili kuchagua viongozi yeye atakapotangaza kujiuzulu rasmi.
“Anaweza kufanya hivyo, yaani kutangaza kujiuzulu na kutangaza
uchaguzi, pia kuwaomba radhi wanachama na mashabiki waliomuunga mkono
muda wote.”
CREDIT- CHAMPION
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: