ads

KATIKA namna isiyotazamiwa kutokea kwenye maeneo mengine nchini, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, wamevaana tena na kupigana vijembe.


Kisa cha kuvaana tena kwa wawili hao, kinadaiwa kuwa siyo kingine isipokuwa ni kutifautiana kwao mtazamo kuhusiana na namna ya kuongoza. Lema anamtuhumu Gambo kuingilia baadhi ya mambo asiyostahili kwa nafasi yake huku Gambo akisisitiza kuwa kamwe hawezi kuyumbishwa na mambo ya kisiasa. 

Tukio hilo ambalo ni mwendelezo wa jingine la aina hiyo lililotokea siku tatu zilizopita, lilijiri juzi na kisha kujirudia tena jana wakati wawili hao walipokutana kwenye vikao muhimu vya utendaji katika mkoa wao.

Oktoba 18, wakati wa kuzindua ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto, itakayojengwa kwa ufadhili wa taasisi ya Martenity Africa, Lema na Gambo walishuhudiwa wakitunishiana misuli baada ya kutofautiana juu ya historia ya mradi huo. 

Jambo hilo lililozua gumzo kubwa, lilitokea wakati Gambo akijaribu kuelezea historia ya kiwanja cha jengo hilo na Lema kumpinga kwa sauti ya juu, akimshutumu kuwa anaupotosha umma kuhusu ukweli wa mradi huo; hali iliyowalazimu polisi waliokuwapo kuingilia kati na kutuliza mambo. 

Juzi, Lema na Gambo walikutana kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) na kuonekana wakiendeleza malumbano yao kwa kurushiana vijembe, kila mmoja kwa wakati wake akimlaumu mwenzake kwa mambo mbalimbali. 

Katika kikao hicho, Lema alikuwa akimlaumu Gambo kwa kuingilia baadhi ya mambo ambayo aliyodai kuwa siyo yake kiutawala huku Gambo naye akijibu mapigo kwa kusema hatakubali kuyumbishwa na mambo ya kisias

Katika kikao cha jana ambacho kilikuwa cha 38 cha Bodi ya Barabara, wawili hao walikutana na kuketi kwa ukaribu zaidi tofauti na juzi baada ya wajumbe wa mkutano huo kumchagua Lema kuwa makamu mwenyekiti huku Gambo akiwa mwenyekiti.

Viongozi hao, ambao licha ya kukaa karibu, kwa muda mwingi walionekana kutochangamkiana wala kuonyeshana sura za bashasha. Hata hivyo, waliendesha vyema kikao hicho, licha ya kwamba Lema alionekana akitoka kabla ya kufikia mwisho.

Haikujulikana mara moja chanzo cha Lema kuondoka kabla ya kikao kufikia mwisho, ingawa wakati akiwamo kikaoni alitoa maoni yake kadhaa ikiwa ni pamoja na kutaka taa ziwekwe kwenye eneo la kona ya Mbauda jijini humo.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: