ads

HARAKATI za aliyekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (Cuf), Profesa Ibrahim Lipumba kutaka kuwania tena kiti hicho, zimeanza rasmi baada ya kiongozi huyo kuibuka katika msiba wa Ismail Mapande 'Kundambanda' na kuonyesha alikusudia kupiga kampeni.


Prof.Lipumba ambaye aliachia ngazi nafasi hiyo wakati Cuf ikijiandaa na Uchaguzi Mkuu wa Desemba 25 mwaka jana, aliibuka ghafla msibani na kutengeneza fursa kadhaa za kuzungumza na waombolezaji kabla na baada ya Kundambanda aliyekuwa mgombea wa ubunge jimbo la Masasi kupitia Cuf kuzikwa.

Kwanza alitambulishwa kuwa mgeni rasmi, wakati aliyepewa nafasi hiyo ni Mkurugenzi wa Sera na Uchaguzi wa Cuf Taifa, Shaweji Mketto ambaye licha ya kuwapo kwake katika tukio, ugeni rasmi ukaelekezwa kwa Prof.Lipumba.

Akuzungumza katika msiba huo, Prof.Lipumba alikiri kuwa licha ya kufanyakazi kwa kipindi kifupi na marehemu Kundambanda, ilitosha kutambua uwezo na ushawishi mkubwa aliokuwa nao kisiasa.

Mwenyekiti huyo mstaafu alitoa sh.50,000 na kuahidi nyingine 150,000 ili zitumike kufungua akaunti maalum ya mtoto wa miaka mitano wa marehemu Kundambanda ili zimsaidie katika elimu mara atakapoanza elimu ya sekondari.

Hata hivyo, wakizungumza katika tukio hilo baadhi ya waombolezaji na wengi wao wakiwa wafuasi wa chama cha Cuf na Chadema, walisema hatua hiyo ya Prof.Lipumba ni mpango wake wa kuanza kushawishi wanachama ili wampigie kura wakati wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Agosti 21 mwaka huu,

Muombolezaji Issa Matandu amesema kuwa Prof.Lipumba hafai tena kuchaguliwa kuwa mwenyekiri wa Cuf kwa sababu alikiteleza chama wakati mgumu na dhamira yake ililenga kuona chama kinakufa kabisa.

credit- Nipashe

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: