![ads](http://1.bp.blogspot.com/-J5aEnGVep5k/WJTrf2fzuPI/AAAAAAAAU5U/_iuE-DY1RHAM5_hqPHb-UuNbabG2xn2nwCK4B/s1600/AdvertiseHere.jpg)
WAKATI wanachama wa Simba wakijiandaa
kuingia kwenye utaratibu wa klabu kuendeshwa kwa mfumo wa kampuni,
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema klabu
hiyo itapata maendeleo iwapo itangia kwenye mfumo huo.
Akizungumza
kwenye mahojiano na kituo kimoja cha radio Dar es Salaam, Nape alisema
kuwa hatua ya kubadili mfumo utaifanya Simba ijiendeshe kisasa na
kuharakisha mafanikio ambayo ndiyo kiu ya mashabiki na wanachama wa
klabu hiyo.
"Mnaweza mkaiondoa klabu na kuipeleka kwenye kampuni, lakini ubabaishaji ukashindwa kuleta maendeleo, ni vizuri hata hao wanaotaka kuwekeza katika mfumo wa kisasa wasiwe wababaishaji, wanatakiwa wawe watu makini," alisema Nape.
Waziri huyo alisema ni vizuri kanuni na taratibu za mfumo huo mpya zikafuatwa ili kuepuka mambo yasiyoitajika ambayo huenda yakavuruga nia njema hiyo.
Wanachama wa Simba wanatarajiwa kufanya uamuzi wa kukubali au kukataa mabadiliko hayo katika mkutano mkuu utakaofanyika Jumapili kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay jijini.
"Mnaweza mkaiondoa klabu na kuipeleka kwenye kampuni, lakini ubabaishaji ukashindwa kuleta maendeleo, ni vizuri hata hao wanaotaka kuwekeza katika mfumo wa kisasa wasiwe wababaishaji, wanatakiwa wawe watu makini," alisema Nape.
Waziri huyo alisema ni vizuri kanuni na taratibu za mfumo huo mpya zikafuatwa ili kuepuka mambo yasiyoitajika ambayo huenda yakavuruga nia njema hiyo.
Wanachama wa Simba wanatarajiwa kufanya uamuzi wa kukubali au kukataa mabadiliko hayo katika mkutano mkuu utakaofanyika Jumapili kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay jijini.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: