ads

WAKATI wanachama wa Simba wakijiandaa kuingia kwenye utaratibu wa klabu kuendeshwa kwa mfumo wa kampuni, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema klabu hiyo itapata maendeleo iwapo itangia kwenye mfumo huo.


Akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja cha radio Dar es Salaam, Nape alisema kuwa hatua ya kubadili mfumo utaifanya Simba ijiendeshe kisasa na kuharakisha mafanikio ambayo ndiyo kiu ya mashabiki na wanachama wa klabu hiyo.

"Mnaweza mkaiondoa klabu na kuipeleka kwenye kampuni, lakini ubabaishaji ukashindwa kuleta maendeleo, ni vizuri hata hao wanaotaka kuwekeza katika mfumo wa kisasa wasiwe wababaishaji, wanatakiwa wawe watu makini," alisema Nape.

Waziri huyo alisema ni vizuri kanuni na taratibu za mfumo huo mpya zikafuatwa ili kuepuka mambo yasiyoitajika ambayo huenda yakavuruga nia njema hiyo.

Wanachama wa Simba wanatarajiwa kufanya uamuzi wa kukubali au kukataa mabadiliko hayo katika mkutano mkuu utakaofanyika Jumapili kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay jijini.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: