ads

MENEJA Mawasiliano wa Hifadhi za Taifa (Tanapa), Pascal Shelutete, amesema wasanii wa filamu nchini wanatakiwa kutumia mandhari za asili zilizoko katika hifadhi za Taifa kwa ajili ya kurekodi filamu zao ili kutangaza utalii wa ndani.


Shelutete alisema hayo katika tamasha la chama cha wasanii wa filamu wa jijini Arusha (TFDAA) katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, akidai kwamba Tanapa itatoa ushirikiano kwa wasanii watakaoonyesha nia ya kurekodi filamu zao katika maeneo ya hifadhi ambayo ni salama na yenye mvuto mkubwa.

“Nchi yetu imejaliwa vivutio vingi hivyo wasanii washirikiane na Tanapa kuutambulisha utalii wetu ili ziweze kuchangia pato la Taifa,” alisema Shelutete.

Naye Rais wa Shirikisho la Silamu nchini (TAFF), Simon Mwakifamba, aliwataka wasanii watumie fursa ya maonyesho ya kimataifa ya filamu yanayojulikana kama Tanzanite International Film Festival yatakayojumuisha wasanii wa filamu kutoka nchi mbalimbali duniani kujitangaza na kutengeneza marafiki wakusaidiana katika sanaa zao.


DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: