
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amesema ndoto ya kutambulika katika medani ya soka duniani inatarajia kutimia muda mfupi ujao.
Nahodha huyo wa timu ya taifa, 'Taifa Stars' alisema hatua ya jina lake kuwemo katika orodha ya nyota 30 wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika mafanikio makubwa.
Majina mengine ya wanasoka wanaocheza Ulaya yaliyotajwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf) ni Mohamed Salah (Misri/Liverpool), Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon/Borussia Dortmund) na Eric Bailly (Ivory Coast/Manchester United).
"Naanza kuona ndoto yangu inaanza kuwa kweli. Ni faraja jina langu kuwemo katika orodha ya washindani," alisema Samatta anayecheza soka ya kulipwa katika klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji.
Mchezaji huyo mwenye miaka 24, alisema kuwa hatua ya kutajwa kuwania tuzo hiyo ni fursa kwa wachezaji wa Tanzania kujifunza.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa TP Mazembe Englebert ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), alisema anatarajia kupata mafanikio Genk.
Samatta, alishindwa kuendelea na mchezo wa Jumamosi, baada ya kuumia katika mchezo waliotoka suluhu na Lokeren hatua iliyoibua hofu kama ataitumikia Taifa Stars dhidi ya Benin.
"Nasubiri taarifa ya daktari wa klabu yangu ndio nitajua kama nitajiunga na Taifa Stars kwa mchezo wetu na Benin au vinginevyo," alisema Samatta.
Taifa Stars inatarajia kujitupa uwanjani ugenini kumenyana na Benin katika mchezo uliopangwa kuchezwa Novemba 11.
Post A Comment: